03/02/2023
KATIKA KILA MAPITO, CHAGUA KUJIFUNZA.
Unapoona changamoto zimekuandama, mapito ni mengi, fahamu kuwa kuna jambo unatakiwa kujifunza. Usikimbilie kulalamika na kuanza maombi yasiyoeleweka. Kaa chini, kisha tafakari.
Mhubiri 7:14, "Siku ya kufanikiwa ufurahi, Na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asipate kulijua neno lo lote litakalofuata baada yake."
Kwanini utafakari? Kutafakari kutakupa hekima ya kuamua, kusema, kumshirikisha mtu sahihi na kuomba. Usiharakishe kufanya jambo lolote kabla ya kutafakari kuhusu jaribu au changamoto hiyo.
MCHUNGAJI VICTOR GASPER MALAMLA - KANISA LA EFATHA NUNDU MWANZA.