29/06/2017
Umewahi kusikia wapi Toyota RV4 au Carina ikajivuna kwa kuwa k**a ilivyo? Umesikia wapi RV4 ikamlingia Carina? Malingo ya uzuri wa Magari hufanywa na mtengenezaji mwenyewe, yeye ndiye anajua gari aina fulani na ranging fulani imetimiza maksudi ya kutengenezwa kwake. Ajuaye kusudi la kutengeneza aina fulani ya gari ni mtengenezaji mwenyewe na huyo hufurahi kila anapoona kusudi lake limetimia.
Inakuwaje wewe unajiuvuna kuwa mwanaume au mwanamke? Inakuwaje unahangaika kujilinganisha na mwanaume au mwanamke mwingine? Umekua mwanaume au mwanamke kwa kusudi la aliyekuumba. Aliyekuumba ndiye anajua k**a unakidhi vigezo vya kuumbwa kwako au la. Inakuwaje unajivunia kuwa mwanaume au mwanamke? Samaki baharini au mtoni anajivunaje kujua kuogelea wakati ameumbwa ili aogelee majini? Samaki ataenda mafunzo ya kuogelea wakati uwezo huo umewekwa mapema na muumbaji mwenyewe? Je mwewe ajajivunaje kwa kujua kuruka angani?
Kuwa mwanaume au mwanamke si kitu cha kujivunia au hata kuhangaika ili kujipatia sifa kwa sababu ya jinsi hizi. Aliyekuumba atajivunia wewe kwa kuishi kusudi la kuumbwa kwako, maono aliyoweka ndani yako, na maono yaliyowekwa ndani yako si ya kuitwa Baba au Mama fulani. Kuwa Baba au Mama hakuongezi ubora wako bali ujue uliumbwa tayari kwa ajili ya hayo.
Ndani ya kuwa mwanaume au mwanamke kuna kusudi ambalo ni tofauti na jinsi zetu na ili kulijua kusudi hilo lazima uombe "how to use/operate manual" kutoka kwa mtengenezaji. Huwezi kujifunza namna ya kutumia jinsi zetu, hizo ni natural readily available for use, ni k**a mwewe arukaye na hahitaji course maalum au samaki aogeleaye Majini.
K**a huombi manual kwa aliyekuumba utakufa na kusudi alilokuumbia bila kuleta faida kwa ulimwengu. Utafananishwa na mwana mpotevu katika simulizi za Biblia.
Thubutu kuishi maisha nje ya maumbile ya jinsi ili talanta yako izae. You are more spiritual than physical appearance.
Uwe na siku njema