04/08/2020
Tuangalie sababu KUBWA zinazofanya computer kuwa nzito katika utendaji kazi na solution zake
1. Ram (random access memory)
hiki ni kifaa au kichochezi muhimu sana katika mfumo mzima wa ufanyaji kazi wa computer ambacho katika ufanyaji kazi huo huambatana na processor na hard disk....Ram inapokuwa ndogo sana husababisha pia uchapaji kazi nao kuwa mdogo.....hakikisha Ram iliyopo kwenye computer yako ni kubwa inayomudu kazi zako na speed ya processor yako at least 4gb
2. Processor (cpu)
part hii ndy ubongo wa computer na ili fanye kazi vizuri lazima kuwe na proper cooling system ambayo itaipooza pale inapofanyakazi kwa muda mrefu na kupata joto sana. computer isipo fanyiwa service kwa muda mrefu inaweza kuiathiri processor km ifwatavyo....vumbi na uchafu wa muda mrefu huziba matundu ya hewa na kufanya feni isifanye kaz km inavyotakiwa na hivyo processor haipati hewa ya kutosha hivyo hupata joto jingi na meishowe inakuwa nzito hata kufeli kabisa.....hakikisha computer yako inafanyiwa service na kusafishwa ipasavyo, hakikisha cooling system ipo sawa matundu hayajaziba na feni ni nzima
3. Hard disk
hii ndy storage ya computer ambapo data zinahifadhiwa, inapokuwa na shida au tatizo hard disk mfano katika 'sector' huweza kusababisha kufeli katika ku read and write data zilizopo katika spinning disk hivyo kuwa nzito .pia storage inapokuwa ndogo hadi kuindicate RED husababisha computer kuwa nzito kwa sababu ya nafasi ndogo au kutokuwa na nafasi kabisa ya kuchakata data!.....hakikisha hard disk ni nzima na inanafasi ya kutosha au blue color indication inatosha avoid red colour!!
hzo ni baadhi ya Sababu KUBWA lakini zipo ndogo ndogo pia....see yu next post