05/09/2024
Acha kuchukua MWANAUME ambaye hana kazi halafu unakuja kumsimanga kuwa hakuhudumii, uliombwa?
Unakutana na kaka wa watu ambaye hana kazi, au ndiye anayeanza kazi au biashara yake ndogo, bado anajitafuta maishani na hajapata mwelekeo. Wewe una kazi nzuri na kipato kikubwa, unamuambia unampenda hivyo hivyo, mapenzi hayachagui pesa. Basi unalazimisha mkae pamoja, na wewe ndiye unayelipa kodi na kutoa kila kitu humo ndani.
Kaka wa watu bado maisha yake hayajajipanga, unalazimisha afanye mambo makubwa k**a kuja kwenu kujitambulisha na kutoa mahari, wakati mwingine hata unajilipia mahari mwenyewe ili tu akuoe. Mnaoana au mnaendelea kuishi pamoja, sasa kaka anafurahia kulelewa, anakula hela zako na hakuhudumii chochote. Unaanza kulalamika, "Mbona hanipi hata mia?" "Mbona hanihudumii chochote?" "Ananipenda kweli?"
Dada, kilikuwa ni kiherehere chako, narudia, ni kiherehere chako, hivyo tulia, amka kutoka kwenye ndoto, usisumbue watu! Nani alikuambia uchukue mwanaume na uanze kumlea? Lini katika kufundwa ulifundishwa utafute mtu ambaye hana pesa na uanze kumsumbua? Kaka wa watu alikuwa anafurahia maisha yake kuishi chumba kimoja cha elfu 20, unakwenda kukodi nyumba nzima unataka kumpa presha alipie kodi ya laki 3.
Mna mtoto, mkaka wa watu hata hana unampeleka mtoto shule ya mamilioni, halafu unalalamika, "Halipi ada," kwani elimu si bure? Uliombwa umpeleke kwenye hiyo shule? Acheni kutia watoto wa watu presha na kuwachokoza kwa kutaka maisha ya juu!
Dada, hujalazimishwa, k**a unataka mwanaume mwenye hela, subiri utafute mwenye hela. Lakini k**a unataka mwanaume ambaye atakusaidia kila kitu, mbona wapo wengi? Lakini kumchukua kijana wa watu anayeanza kujitafuta halafu unataka aishi maisha yako, kumsimanga kila siku kuwa hahudumii kumbe ni shida zako, itakula kwako!
NB; Mwanume acha kupenda kulelewa utadhalilika, jitume hata k**a huna kihivyo toa hata kidogo, rudi hata na NDIZI nyumbani ulinde unaume wako!