06/12/2023
Jana December 5, 2023 ilikua ni Siku ya Kujitolea kimataifa kufanya kazi bila ya Malipo katika sekta ya kiuchumi na maendeleo ya Kijamii “Economic Sector and Social Development “ Je umewai kujitolea au kufanya jambo lolote Lile bila ya kutegemewa kulipwa ili unachofanya kiwe ni kwa faida ya watu waliokuzunguka na Jamii yakoo kwa Ujumla?
Mimi na Marafiki zangu kwa namna moja au nyingine tumekua tukitenga mda wetu kidogo na kujitoa japo kwa uchache kwa ajili wa Wengine. matamanio yetu siku zote imekua ni kuona tunapata mabadiliko chanya kwenye changamoto mbalimbali ambazo zinaiikabili Jamii yetu. Binafsi safari yangu ya kujitoleaa ni ya takribani miaka kumi sasa kuanzia kule Muungano Secondary nikitumia sanaa ya uandishi. Baadae pale chuo kikuu cha Iringa nikiwa kwenye Asasi Mbalimbali ndani ya Chuo na Zingine nje ya Chuo
2014 tulikua kule Iramba kwa Mwigulu Nchemba tukisaidia Mradi wa Maji na Afya, nakufundisha mashuleni namna ya kutumia rasilimali zinazowazunguka kutengeneza vitu ambavyo vinaweza kurahisisha maisha yao k**a vile majiko ya kisasa, baadae tukaenda Ndala Shinyanga na Bariadi katika mradi wa Watoto chini ya Shirika la Save the Children wakishirikiana na Raleigh international
Kwa kujitolea nimehudumu kwenye Asasi mbalimbali kwa namna moja au nyingine kwa kufanya kazi bila ya malipo K**a Raleigh Tanzania wakishirikiana na Restless Development na VsO, Raleigh Tanzani Societ, Save the Children, World Merit, Tengeneza Generation Kule Gifted Heart Kaka Mkubwa Malisa GJ ametuongoza vyema sana kujitoa kwa kiasi chetu kwa watu mbalimbali na bado anafanya kazi nzuri sana kwa kugusa jamii kwenye nyanja nyingi k**a ambayo juzi imeongora hamasa ya kuchangia Damu kwa wakazi wa Dodoma
Pia Kuna hatua nyingi tumechukua na marafiki zangu na watu wanaonizunguka hapa Kariakoo k**a vile kuchangisha fedha kwa ajili ya matibabu ya watoto, Chakula cha Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, na fedha kwa ajili ya vitabu mbalimbali amabvyo vitawasaidia kwenye masomo na harakati zao, yapo mengi japo kuyakumbuka yote kwa Pamoja inaweza kua ni ngumu
Kwenye kujitolea kuna changamoto k**a ilivyo sehemu nyingine za kazi za malipo lakin swali moja ambalo linatutatiza kila wakati baadhi ya watu wasipojitoa kwa ajili ya wengine wasio na uwezo wa kupaza sauti juu ya yale yanayowatatiza nani atafanya hivyo? Watoto na watu wengine ambao wanakua wamekata tamaa huku wanapigania afya zao kitandani nani atafanya hivyo? Kuna watoto yatima na walio kwenye mazingira magumu wakati mwingine wanakosa ada na chakula kukiwa hakuna mtu wa kuwasemea nani atafanya hivyo…
Changamoto za Kujitolea ni nyingi wakati mwingine watu wengi wanadhani ili ujitolee kusaidia kundi flan kwenye Jamii pengine unapaswa kua hauna shuhuli maalumu ya kufanya Dhana hii inapaswa kubalika haiendani kabisa na Lengo na Kujitolea kwa jamii yako kwa kua lengo la kujitolea ni kuchochea mabailiko chanya kwenye Jamii. Ukiona mema ya kujitolea na faida zake kwa wahusiika basi utapata nguvu ya kuendelea kujitolea bila kujali unapitia changamoto gani…
Kujitolea sio sehemu ya kutafuta Sifa au kujikweza ni sehemu ya Kutatua changamoto za Watu. Helen Dyer anasema Kujitolea ni Kufanyia kazi vilio vya watu kwa matendo. Matendo haya yanaweza kuharakisha matokeo chanya kwenye jamii yako. Mwaka huu December 2023 mimi pamoja na Marafiki zangu hapa Kariakoo tumejitolea kukusanya Fedha kwa Ajili ya Watoto wanaozaliwa na Mgongo wazi na Vichwa vikubwa, fedha hizi zitaelekezwa moja kwa moja kwenye matumizi ya BIMA ya Afya…
Binafsi niwapongeze watu wote ambao mmekua mstari wa mbele kusaidia wasio na sauti, wenye uhitaji, mmetenga mda wenu na kuutumia kwa ajili ha wengine Baba yenu wa mbinguni atwalipia kazi jii ambayo mnaifanya kwa mioyo yenu bila kuwaza kabisa namna mtakavyonufaika nawatakia maandilizi mema ya Xmass na Mwaka Mpaya 2024
Nawasilisha Ndahani N. Mwenda Happy Wa Joseph Christopher Cyrilo