21/10/2020
Zijue faida za Kula ndizi;
Ndizi ni Tunda linalofahamika kwa wingi wa virutubisho na madini mengi zaidi k**a vile Potassium, Vitamin C pamoja na Vitamini B6
Faida zake:
1. Ndizi mbivu ni chanzo kizuri cha Vitamini C , huweza kutoa
kiwango cha vitamini C Kinachohitajika kwa siku.
2. Huboresha afya ya moyo na kukukinga zaidi dhidi ya
ugonjwa wa kupooza inajulikana k**a Stroke.
3. Husaidia kuboresha afya ya Figo na kulifanya liweze kufanya kazi
vizuri.
4. Husaidia kukufanye kuhisi kushiba baada ya mlo, hii kwa watu
wa diet kukuepusha kula kula mara kwa mara.
5. Huthibiti kiwango cha sukari mwilini
6. Husaidia katika mfumo wa umeng'enywaji wa chakula na
kudhibiti tatizo la kupata choo kigumu kitaalamu k**a
constipation, hali hii huwapata watoto wadogo pamoja na watu
wazima
7. Huboresha na kuchangamsha akili na kukutoa katika msongo
wa mawazo
8. Huweza kusaidia katika swala zima la kupunguza uzito basi
tunda hili liliwe kwa kiasi kwa kuzingatia lishe bora.
Kuendele kupata ndondoo hizi juu ya faida za chakula ama matunda mbalimbali tufuatilie katika ukurasa wetu wa
Smart Growth Diary- SGD
Je ungependa kujua faida ya Chakula gani? Tujulishe kupitia comment hapa chini.