04/07/2022
JINSI YA KUPATA SIMU ILIYOPOTEA
Makala Hii Imetolewa Na: Phidtech Ict Solutions,July 2022.
Ni Jambo la Muhimu kuhifadhi IMEI namba ya simu yako inayopatikana kwenye karatasi zilizomo kwenye box la simu uliyonunua au nyuma ya Simu unapotoa mfuniko wa nyuma ya Simu.IMEI namba inaweza kuwa zaidi ya Moja Kutegemea na leini za simu zinazoruhusiwa kwenye simu Yako.Kama simu inaruhusu leini za simu mbili ivyo utakuta IMEI namba mbili.IMEI namba ni muhimu kwa sababu hii ni sawa na namba ya utambulisho ya simu yako ndio maana ni muhimu kuwa nayo pembeni au sehemu salama.
👉Jinsi ya kupata simu iliyopotea kwa kutumia IMEI
Kwasasa zipo programu nyingi sana zinazodai kuwa zina uwezo wa kupata simu iliyopotea kwa kutumia IMEI namba, lakini sio za kuaminika kwa asilimia 100.
Changamoto ni kuwa zipo apps Play Store kwajili ya kutoa huduma hii nyingi na zinalalamikiwa kwa kutofanya kazi kwa usahihi.
👉Njia ya Kupata Simu Iliyopotea Tunayopendekeza
Hakikisha unatoa taarifa polisi kwani hapa Tanzania Sasa kuna kitengo cha cyber crime ambacho kipo kwenye kila kituo cha polisi ambacho kitengo hiki ushirikiana na TCRA kwaajili ya kutoa huduma kwa wananchi. Hivyo basi hatua ya kwanza ni toa taarifa polisi na hakikisha una IMEI namba au risiti ya simu iliyopotea.
👉Unaweza pia kuwasiliana na kampuni ya kutoa huduma za simu uliyokuwa unatumia kabla ya simu yako kuibiwa, hakikisha unakuwa na IMEI ya simu yako kabla ya kutoa taarifa.
👉Kama Bado haujafanikiwa unaweza kutumia programu mbalimbali za kupata simu iliyopotea kwa kutumia IMEI, Unaweza kujaribu hatua hii k**a hatua tulizoa apo juu hazijafanikiwa mfano wa Programu hizi ni k**a vile Find my device nk