09/02/2020
JE ACCOUNT ZAKO ZA MITANDAO YAKIJAMII NA NYINGINEZO HUWA UNAZIWEKEA ULINZI WAKUTOSHA?
Kila mtu huwa anajiuliza nawezaje kuweka ulinzi kwenye account zangu k**a instagram na nyinginezo?.......
kimsingi vyote hivyo vinakuwa controlled na e-mail yako, k**a unatumia android automatic utatumia Gmail account na mtu akiweza kupata hiyo email yako anaweza aka-access vitu vyako vya private k**a meseji picha na vingine.....
Ndio maana unasikia mara mtu amehack (amedukua) account yako ya insta, facebook or whatever.....basi ujue alipata email or password yako na anaweza kucontrol kila sehemu ambapo umelink hiyo email though sasa hivi kuna technique nyingi sana zaku-hack naku-access account mbali mbali watu wanahack mpaka data za siri za serikali ya marekani k**a ushawahi kusoma au kusikia ile scandal ya Edward Joseph snowden ambayo nilishawahi kuipost before....
Hakuna kitu chakuzingatia na cha msingi k**a security (ulinzi) unapotumia simu au computer au vitu vinavyofanana na hivyo.......
mfano iphone wanakitu kinaitwa advertising ukiwa umekiruhusu (allow) kwenye simu yako utakuta ukiingia kwenye site mbali mbali unaanza kuona matangazo mbali mbali ambayo yanaendana na vitu unavyopenda sababu washajua vitu ambavyo unapenda sana kuvifatilia........
Dunia sasaiv imepiga sana hatua kutokana na utandawazi so unapotumia hivi vifaa vya teknolojia ya computer zingatia sana kitu kinachoitwa SECURITY (ULINZI)..
Jitahidi sana kuwa unabadilisha password ya account zako kila baada ya muda fulani pia usijaribu kutumia password moja kwenye kila account....
Mfano wengine wanatabia yakutumia password moja kwenye Facebook, instagram Twitter, Gmail, Yahoo n.k hii yote nikuepuka kusahau lakini ni hatari sana kwa usalama wa account zako....
Cha mwisho jitahidi sana unapotengeneza password tengeneza password ngumu kuing'amua epuka kutumia namba tupu au maneno tu, jitahid kuchanganya maneno, namba na characters nyengine k**a #$%@! Itakusaidia sana...
Be big than your biggest fear, adios amigo ciao 👊