26/10/2017
MAMBO KUMI YANAYOWEZA KUONGEZA USALAMA WA TAARIFA ZAKO MTANDAONI
Tunapotumia mtandao zipo taarifa nyingi tunazozihifadhhi, na ni muhimu sana kuzingatia usalama wa hizo taarifa.. hasa zile taarifa zetu za siri.
Zifuatazo ni njia kumi zitakazokusaidia kuongeza usalama wa taarifa zako ulizozihifadhi mtandaoni.
1. Usitumie ‘Nenosiri’ (password) zinazofanana kwenye mitandao tofauti au akaunti tofauti (mf. Gmail na facebook account).
------------------------------------------------------------------------------------
Watu wengi huwa wanajikuta wana nenosiri moja ambalo huwa wanapenda kulitumia kwenye kila akaunti k**a vile Gmail, facebook na twiter. Hii sio nzuri hata kidogo, kwa sababu k**a mtu akifanikiwa kulijua basi anaweza akaingia kwenye akaunti zako zote za mtandaoni. Hakikisha unatumia Nenosiri tofauti kwa kila akaunti unayofungua mtandaoni.
2. Usimwambie au usimpe mtu neno lako la siri (au password yako) na badilisha mara kwa mara.
--------------------------------------------------------------------------------------
Watu wengi huwa wanajikuta kwa namna moja au nyingine wanaweka wazi taarifa ambazo zinapaswa ziwe siri, mfano nenosiri (au password zao), hii inawaweka kwenye hatari ya kuwapa watu wengine uwezekano wa kuingia kwenye akaunti zao muda wowote wanaotaka na kuona taarifa zao na mbaya zaidi hata kuzibadilisha au kuzifuta kabisa. Hakikisha neno lako la siri (au password yako) linabaki kuwa siri yako. Pia hakikisha unabadilisha nenosiri mara kwa mara.
3. Epuka kutumia huduma za mtandaoni ambazo hauna uhakika k**a ziko salama.
--------------------------------------------------------------------------------------
Mara nyingi tunapotumia mtandao huwa tunakutana na ofa mbalimbali ambazo zinawekewa maneno k**a “bofya hapa” au “Click here”. Hakiisha unakuwa makini sana na kile unachobofya, maana kwa kubofya unaweza ukajikuta unajiinghiza kwenye hatari ya kuzikabidhi taarifa zako kwenye mikono ya watu wabaya. Uwe makini.
4. Epuka kutoa taarifa zako za muhimu mfano anuani ya barua pepe (email address), nambari ya akaunti ya ya benki kwenye tovuti au kwa mtu ikiwa hauna uhakika k**a ni salama kufanya hivyo.
--------------------------------------------------------------------------------------
Inawezekana umeshawahhi kujaribu kupakua kitu mtandaoni na wakakudai barua pepe yako, au umeshawahi kutumiwa ujumbe wa facebook au mitandao mingine na mtu usiyemjua na akahitaji umtumie barua pepe yako ili muendelee kuchati au ili akutumie picha zake, au muda mwingine kuombwa uingize taarifa zako za kibenki. Ni muhimu kukumbuka kuwa taarifa zako ni za muhimu, na sio kila mtu anaweza akawa nazo, hivyo epuka kuzitoa ikiwa hauna uhakika k**a ni salama kuzitoa.
5. Jitahidi kuwa na muda wa kujifunza kuzitumia huduma mbalimbali za mtandaoni, usipende kufanyiwa kila kitu.
--------------------------------------------------------------------------------------
Mara nyingi kuna watu ambao huwa tunapenda wawepo watu wengine wa kutusaidia kufanya baadhi ya vitu mtandaoni mfano kufungua akaunti mbalimbali za mtandaoni, au kupata huduma zingine za mtandaoni. Na mara nyingi hivyo vitu wanavyotusaidia kufanya hata sisi tungeweza kuvifanya endapo tungepata muda mfupi tu wa kujifunza. Na mara nyingi shida inatokea pale ambapo hii kazi ya kutusaidia kufanya vitu mtandaoni inapoangukia mikononi mwa mtu ambae si mwaminifu.
K**a bado una uwezo jitahidi kutoa muda wako kujifunza kufanya mwenyewe na sio mtu mwingine akufanyie, hii itaongeza usalama wa taarifa zako.
ITAENDELEA………………….
…… …….