Rafiki TZ

Rafiki TZ Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Rafiki TZ, Internet Company, Dar es Salaam.

Ni wengi wanaoutumia na kuufahamu mchaichai k**a kiungo cha chakula jikoni na wengine hutumia k**a dawa ya mbu. Lakini, ...
23/08/2016

Ni wengi wanaoutumia na kuufahamu mchaichai k**a kiungo cha chakula jikoni na wengine hutumia k**a dawa ya mbu. Lakini, je unafahamu kuwa majani haya yana faida kubwa kiafya . Mafuta ya mchachai hutumika katika viwanda vinavyotengeneza pafyumu na sabuni.
Tafiti kadhaa zinaonyesha kuwa mchaichai una vichocheo muhimu vinavyoweza kupambana na athari kadha wa kadha tumboni, kwenye mkojo na hata kwenye vidonda.
Watu wengine huamini kuwa mchaichai unaweza kutibu baadhi ya maradhi k**a vile homa ya matumbo, matatizo ya ngozi, madhara yanayotokana na ulaji wa chakula chenye uchafu na pia hutibu maradhi ya kichwa na hata misuli. Mchaichai pia unatajwa kuwa kinywaji kinachoweza kupunguza joto. Chai ya mchaichai inasaidia kupunguza joto kwa mgonjwa wa homa. Faida nyingine za mchaichai kiafya ni pamoja na Kinga dhidi ya saratani.

RAIS John Magufuli ameiagiza Bodi ya Pamba Tanzania (TCB) kuhamia katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na kuondoka Dar es Salaa...
01/08/2016

RAIS John Magufuli ameiagiza Bodi ya Pamba Tanzania (TCB) kuhamia katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na kuondoka Dar es Salaam, kwa sababu huko ndiko ambako wakulima wengi wa zao hilo wanapatikana.

Aidha, ameionya bodi hiyo kwamba hataki kusikia kwamba imetoa tena mbegu zisizoota kwa wakulima, na endapo hilo litatokea, atawatumbua viongozi wake.

Rais Magufuli aliyasema hayo mjini Geita wakati akizungumza na wananchi, akiendelea na ziara zake katika mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Geita, ambayo aliianza mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mtoto wa miaka 7 ameaga dunia katika mazingira ya kustaajabisha sana.Amini usiamini msichana huyo mwenye umri wa miaka 7...
29/07/2016

Mtoto wa miaka 7 ameaga dunia katika mazingira ya kustaajabisha sana.
Amini usiamini msichana huyo mwenye umri wa miaka 7 amepigwa jiwe na ndovu!
Tukio hilo la ajabu lilitokea katika hifadhi ya wanyama mjini Rabat Morocco.
Ndovu huyo alipura jiwe juu ya ua linalozunguka hifadhi hiyo na kwa bahati mbaya likampata mtoto huyo.
Msichana huyo alipelekwa hospitalini lakini akaaga dunia muda mchache baadaye.
Katika taarifa kwa wanahabari wasimamizi wa hifadhi hiyo wametuma rambirambi zao kwa familia ya marehemu na kusema kuwa hilo lilikuwa tukio la kipekee kwani ua huo umetimiza vigezo vyote vya kimataifa ila hio ilikuwa ni ajali tu.

Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Japan umethibitisha kwamba kukaa kwa mda mrefu na kutazama vipindi vya televisheni ...
28/07/2016

Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Japan umethibitisha kwamba kukaa kwa mda mrefu na kutazama vipindi vya televisheni kwa masaa mengi kunahatarisha afya kwani huhusishwa na maradhi yanasababisha mzunguko wa damu mwilini kutokuwa sawa.
Watafiti hao wanasema, hali hiyo pia huenda ikasababisha damu kuganda na kutengeneza vidonge katika sehemu k**a vile miguu, na iwapo mgando huo utasukumwa na nguvu za mzunguko wa damu na kuingia sehemu k**a vile mapafu, husababisha vifo.

Paulina Mgeni ni Mwanamitindo (Model) anaefanya kazi za urembo na maonesho ya mitindo kwa kujitegemea yeye mwenyewe hayu...
23/07/2016

Paulina Mgeni ni Mwanamitindo (Model) anaefanya kazi za urembo na maonesho ya mitindo kwa kujitegemea yeye mwenyewe hayupo chini ya kampuni yoyote wala chini ya lebo ya mtu yeyete, japokua amekuwa akifanya shoo nyingi kwa kushirikiana na baadhi ya makampuni na wabuni mbalili, kwasasa anatafuta Meneja wa kuwa anamsimamia kazi zake.
Paulina Mgeni ndio Miss Utalii Mkoa wa Iringa mwaka 2013 mpaka sasa kabla mashindano hayo hayaja simamishwa; ila kwasasa anafanya kazi za mitindo akiwa k**a Mwanamitindo (Model), lakini anahitaji meneja wa kusimamia kazi zake hizo za Urembo (Modeling).

Magari yasiyotumia mafuta yameanza kuuzwa na kutumiwa nchini Kenya kwa mara ya kwanza. Takriban watu watano sasa wanajiv...
23/07/2016

Magari yasiyotumia mafuta yameanza kuuzwa na kutumiwa nchini Kenya kwa mara ya kwanza. Takriban watu watano sasa wanajivunia kumiliki gari hilo.
Magari hayo yanatumia umeme pekee.
Francis Romano, msimamizi wa kampuni inayohamasisha watu magari hayo, anafafanua kuhusu teknolojia hiyo kwa ni mapinduzi katika teknolojia ,,, Je sisi Watanzania tufanyeje ikiwa watu wenye ubunifu k**a huu wanapigwa marufuku

GARI LA NYAYO   Gari la Nyayo ilikuwa mradi wa serikali ya Kenya wa kupanga na kutengeneza magari ya Kenya.Mradi huu uli...
18/07/2016

GARI LA NYAYO

Gari la Nyayo ilikuwa mradi wa serikali ya Kenya wa kupanga na kutengeneza magari ya Kenya.Mradi huu ulianzishwa mwaka 1986 wakati rais Daniel Arap Moi aliomba Chuo Kikuu cha Nairobi kutengeneza magari.Majaribio matano yalifanywa yaitwayo Pioneer Nyayo Cars na yalikuwa na kasi ya 120 km/h. Shirika la magari la Nyayo liliundwa ili kuzalisha magari haya kwa wingi.Hata hivyo, kutokana na ukosefu wa fedha, magari haya hayakuingizwa katika uzalishaji.Shirika la magari la Nyayo baadaye lilipewa jina la Numerical Machining Complex Limited, shirika la kuunda viungo vya chuma vya viwanda vingine.

Kwa wale watumiaji wa simu za Tecno tayari utakuwa unafahamu matoleo ya Camon ambayo lengo lake kuu ni kumuwezesha mtumi...
14/07/2016

Kwa wale watumiaji wa simu za Tecno tayari utakuwa unafahamu matoleo ya Camon ambayo lengo lake kuu ni kumuwezesha mtumiaji wa simu hizo kupiga picha nzuri na za kuvutia hata kwenye mwanga mdogo. Tecno Camon C9 ipo tofauti kidogo kwani imekuja na teknolojia ya lens ya F 2.0 ambayo inawezesha mwanga mwingi zaidi kuingia katika kamera na kufanya picha ziwe na mwonekano mzuri zaidi huku ikiwa na Flash mbili ili kuongeza kiasi cha mwanga huo. ecno Camon C9 imepakiwa katika kasha zuri la rangi ya bluu na nyeusi ambalo kwa juu lina picha k**a ya lens ambayo ni logo ya matoleo ya Camon.

Klabu ya Manchester United ya nchini Uingereza imeorodheshwa ya tano kwa utajiri duniani na jarida la Forbes, thamani ya...
14/07/2016

Klabu ya Manchester United ya nchini Uingereza imeorodheshwa ya tano kwa utajiri duniani na jarida la Forbes, thamani yao ikiwa imepanda kwa asilimia saba. Klabu ya NFL, Dallas Cowboys, ndiyo inayoongoza thamani yake ikiwa $4bn (£3.03bn), na ni mara ya kwanza kwa klabu ambayo haichezi kandanda kuongoza katika orodha hiyo tangu kuanzishwa kwake 2011. United, walioongoza orodha hiyo 2011 na 2012, wana thamani ya $3.32bn (£2.52bn). Real Madrid ni wa pili kwa $3.65bn (£2.77bn) na Barcelona wa tatu $3.55bn (£2.69bn). United, klabu pekee ya Uingereza katika orodha hiyo, walisaidiwa sana na mkataba wao wa £750m na Adidas, jambo lililoongeza thamani yao licha ya kushindwa kufuzu kwa michuano ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. Hata hivyo, Manchester United, ndio wenye deni kubwa zaidi miongoni mwa klabu zilizo katika 25 bora.Arsenal (23), Manchester City (28), Chelsea (36) na Liverpool (41) ndizo klabu hizo nyingine za Uingereza zilizofanikiwa kuwa kwenye orodha hiyo..

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Arsenal Thierry Henry ameondoka baada ya kukataa nafasi aliyopewa ya kufundisha wachezaji...
13/07/2016

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Arsenal Thierry Henry ameondoka baada ya kukataa nafasi aliyopewa ya kufundisha wachezaji wa chini ya umri wa miaka 18. Henry, 38, alipewa nafasi hiyo na meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ambaye alimuambia kuwa hawezi kuchanganya na kazi yake ya sasa k**a mchambuzi wa soka kwenye TV. Hata hivyo, Henry ambaye alifanya kazi na wachezaji chipukizi wa Arsenal k**a sehemu ya mafunzo ya kupata leseni yake ya ukocha ya Uefa, hakuwa tayari kuacha kazi yake ya uchambuzi wa soka. Thierry Henry ameajiriwa na shirika la utangazaji la Sky Spors, na alifanya kazi k**a mchambuzi wa BBC wakati wa michuano ya Euro 2016.

K**a ilivyokuwa mwaka jana lugha ya javascript imeendelea kuongoza katika listi ya lugha za programing zinazotumika kute...
13/07/2016

K**a ilivyokuwa mwaka jana lugha ya javascript imeendelea kuongoza katika listi ya lugha za programing zinazotumika kutengeneza mifumo tofauti ya kompyuta na baadhi ya vifaa vya umeme k**a simu, saa na TV. Ikifuatiwa na SQL Server, Java na C #. Stack Overflow ni mtandao unaowakutanisha madeveloper (watengenezaji) wa programu tofauti duniani, ni sehemu wanayoulizana maswali na kushare idea walizo nazo katika kipengere cha lugha za kompyuta na mifumo yake. Kila mwaka mtandao huo hufanya survey kwa madeveloper kutoka katika nchi 173 duniani kote na kutoa matokeo ya utafiti wao. Mwaka huu madeveloper 56,033 kutoka nchi 173 walishiriki katika utafiti huo na lugha ya javascript kuibuka kidedea ikifuatiwa na SQL Server na Java katika nafasi inayofuata. Mwezi wa kwanza mwaka huu pekee zaidi ya madeveloper milioni 45 walitembelea mtandao huo

Rais wa Ureno Marcelo Rebelo de Sousa ameikaribisha nyumbani timu ya taifa huku wakiambatana na Maelfu ya mashabiki wa t...
12/07/2016

Rais wa Ureno Marcelo Rebelo de Sousa ameikaribisha nyumbani timu ya taifa huku wakiambatana na Maelfu ya mashabiki wa timu hiyo walikusanyika katika uwanja wa ndege mbele ya kasri ya Rais ,na katika mitaa ya mji mkuu Lisbon kusheherekea ushindi wa michuano ya Euro 2016. Nahodha wa timu hiyo Cristiano Ronaldo alilipeleka kombe hilo kwenye kasri ya Rais kabla ya kuanza kulitembeza katika mitaa ya jiji la Lisbon wakiwa katika gari la wazi.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rafiki TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share